NEWS

7 Juni 2017

Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda ya Dar es salaam chaendelea na msako mkali kudhibiti madereva bodaboda na abiria wanaovunja sheria


 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda ya Dar es salaam  Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Awadhi Haji  (gwanda la kijani) amendelea kutoa  elimu kwa madereva wa bodaboda pamoja na abiria ambao wamevunja sheria za makosa ya usalama barabarani ikiwemo kutokuvaa kofia ngumu,bkupita taa nyekundu,bkupakia abiria zaidi ya mmoja na kadhalika. Watuhumiwa wamekamatwa sehemu mbalimbali wilayani Temeke katika msako mkali unaoendelea katika mkoa wa Dar es salaam.
 Watuhumiwa waliokamatwa sehemu mbalimbali wilayani Temeke katika msako mkali unaoendelea katika mkoa wa Dar es salaam wakimsikiliza Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda ya Dar es salaam  Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Awadhi Haji