NEWS

6 Juni 2017

Rais Magufuli: Msimamo Wangu wa Kutoteua Upinzani Bado Upo Palepale..!!!


Rais Magufuli akiongea baada ya kumuapisha Anna Mghwira kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro alisema kuna watu wanahoji alikuwa amezungumza hatoteua wapinzani amesema watu wanatakiwa waelewe alikuwa anazungumza katika maeneo gani, 

Amesema alizungumza akiwa Zanzibar na msimamo wa kutoteua mbunge wa upinzani kutoka nafasi 10 za ubunge upo pale pale na ameshateua 9 bado nafasi moja

Amesema wapo watakaomuonea wivu kutoka CCM, Chadema kwa sababu hakuchagua huko japo wengi wanamuomba omba ila anataka upinzani uwepo