NEWS

26 Februari 2018

Dogo Janja Adaiwa Ameolewa..

Mkali wa Bongofleva Edu Boy ameamua kumjibu Dogo Janja ile kauli aliyomuambia kuwa yeye ni mtoto na kumuambia kwa kusema Janja ameolewa na ndo maana anaona wenzake wadogo hivyo apambane na ndoa yake.

Akiongea na eNEWZ amesema kinachomsumbua Dogo Janja ni kwamba ameolewa na hajaoa, huenda baada ya yeye kufunga ndoa anahisi kwamba kila kitu kipo sawa kwake na kuwaona wasanii wenzake wadogo kiumri na hata kimaisha.

''Dogo Janja ni mdogo sana kwangu kiumri nina uwezo wa kumshika na kumpiga vibao kama mdogo wangu na akatulia asiniambie chochote, kumuoa Irene asione kama amemaliza kila kitu'', amesema.

Edu Boy pia amefunguka kuwa anasikia Stamina anamtafuta hivyo aende tu kwenye maeneo ambayo anapatikana kama studio za Mona Ganster atamkuta wamalizane.
Zaidi fuatilia ENEWZ ya EATV saa 12:00 jioni.