KUFUATIA kifo cha aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT), Akwilina Akwilini ambaye mwili wake umeagwa leo katika viwanja vya chuo hicho na kusafirishwa kwa mazishi, Global Publishers imeshafika nyumbani kwao na marehemu wilayani Rombo-Mashati na kushuhudia maandalizi ya kaburi ambamo atazikwa marehemu.
Maandalizi ya kuchimba kaburi hilo yamefanywa na ndugu na jamaa katika shamba la makaburi ya familia yao yaliyopo kijini kwao.
Global Publishers na Global TV Online inatoa pole kwa ndugu, marafiki, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba wa Akwilina.
Mwenyezi Mungu ailaze mahali pema peponi roho yua marehemu. AMEN!
PICHA NA GLOBAL PUBLISHERS RIPOTA, ROMBO
Tazama video. ya kuaga.
The post Hapa Ndipo Atakapozikwa Akwilina appeared first on Global Publishers.