NEWS

14 Machi 2018

Sakata la Mwanafunzi wa UDSM Kujiteka...Lazidi Kuzua Utata...Taarifa ya Kamanda Mambosasa Yatofautiana na Kamanda wa Polisi Iringa

Kamanda wa Polisi Dar, Lazaro Mambosasa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire wameonekana kutofautiana kimaelezo katika kuelezea sakata la kutoweka kwa Mwanafunzi wa UDSM na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi, Abdul Nondo...

Hapo awali, RPC Bwire alieleza kuwa kijana Abdul Nondo alifika katika kituo cha Polisi Wilayani Mafinga na kuelezea kuwa ametekwa na watu wasiojulikana

Naye RPC Mambosasa, hapo jana alieleza kuwa Polisi Kanda Maalumu ya Dar ililetewa taarifa kutoka Polisi Iringa kuwa Abdul Nondo alipatikana Mafinga akiwa mwenye afya njema na akiendelea na shughuli zake za kawaida na hakuripoti mahali popote si kwa Mwenyekiti wa Mtaa, Mtendaji wa Kata, wala Polisi.