Rais John Magufuli jana alimtumia salamu za heri ya siku ya kuzaliwa, mchungaji maarufu wa Nigeria, TB Joshua, aliyefikisha miaka 55.
Rais Magufuli alituma salamu hizo kwenye ukurasa wake wa twitter, Juni 12 akisema:
“Kwa niaba ya familia yangu, ninatuma salamu zangu za dhati katika siku yako ya kuzaliwa unapotimiza miaka 55. Mungu aendeelee kukupa uongozi mkubwa ili uweze kuleta ukombozi kwa watu wengi na kueneza harufu yake katika mataifa yote.” Heri ya siku ya kuzaliwa.”

