NEWS

24 Agosti 2018

Diwani Mwingine CHADEMA Atimkia CCM.....Sababu ni Serikali Kununua Dreamliner, Kuhamia Dodoma

Uamuzi mgumu wa Rais John Magufuli wa kuboresha usafiri wa anga nchini kwa kununua ndege kubwa ya Boeing 787-8 Dreamliner, umemkimbiza Diwani wa Chadema katika Kata ya Ndumeti, Wilaya ya Siha, Jackson Rabo kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) leo mchana.

Kwa mujibu wa diwani huyo moja ya sababu iliyomvutia kujiunga na CCM baada ya uamuzi wa Rais John Magufuli kuhamishia ofisi zote za serikali mkoani Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Valerian Juwal amethibitisha kuwa Diwani Jackson Rabo anakuwa Diwani wa tano katika wilaya hiyo kujiuzulu mwaka huu.