NEWS

17 Agosti 2018

Tofauti Kati Ya Madeni Ya Ukoo Na Vifungo Vya Ukoo

Ni vigumu  sana  kutofautisha  kati  ya  madeni  ya  ukoo  na  vifungo  vya  ukoo   lakini katika  makala  haya  nitaelezea  tofauti  kati  ya  madeni  ya  ukoo  na  vifungo  vya  ukoo.

MADENI   YA   UKOO   NI   NINI   ?
Madeni  ya  ukoo  ni  mapigo  ambayo  huwapata  watu  wa  ukoo  fulani  kwa  sababu  mababu  wa  ukoo  huo  walivunja  maagano  waliyo  ingia  na  mizimu au miungu wa  ukoo.

Mababu  wa  ukoo  walipoingia  katika  maagano  na  mizimu  wa  ukoo  walipewa  masharti  ambayo  walitakiwa  kuyafuata  na  miiko  ambayo  hawakutakiwa  kuivunja.

 Lakini  baada  ya  kuvunja  maagano  hayo  mizimu  wa  ukoo  huo  waliachilia  mapigo  kwa  watoto  wa  mababu  hao  pamoja  na  vizazi  vyao  vyote.

Haya  ni  mapigo  ambayo  kila  mtoto  anaezaliwa  katika  ukoo  huo  ni  lazima  ayapate. Mapigo  hayo  yanaweza  kuwa  maradhi kama  vile  pumu, kifafa, kisukari  nakadhalika.

Yanaweza  kuwa vijana  wa  ukoo  Fulani  kufa  mapema nakadhalika  nakadhalika.

Mbali  na  kuvunja  maagano  ya  ukoo, madeni  ya  ukoo  pia yanaweza  kusababishwa na  maapizo  yaliyo fanywa  na  mwanaukoo  dhidi  ya  ukoo.

Kwa  mfano  kuna  kisa  kimoja  maarufu  kuhusu ukoo  mmoja  unao  toka  katika  mkoa  mmoja uliopo  hapa  hapa  nchini  Tanzania.

Mababu  wa  ukoo  huo  walikuwa  na  dada  yao  mmoja  ambae  alikuwa  mgumba.

 Dada  yao  huyo  alinyanyaswa  sana  na  wana  ukoo  kwa  sababu  ya  hali  yake  ya  ugumba.

Manyanyaso  yalipo mzidi alienda  hadi  kwenye  eneo yalipo makao makuu  ya  mzimu  wa  ukoo  huo  na  kujiapiza  kwa  uchungu mkubwa  sana  kwamba “ KWA VILE   WANA  UKOO  HUO WAMEMTENGA  NA  KUMNYANYASA  KWA  SABABU  YA  YEYE  KUWA  MGUMBA, BASI HAKUNA  MTOTO  YOYOTE  WA  KIKE  ATAKAE  ZALIWA  KATIKA  UKOO  HUO  AMBAE ATAKUJA  KUBEBA  UJAUZITO  AU  KUZAA  MTOTO”

Alivyo  maliza  kufanya  maapizo  hayo  mwanamke  huyo  alijitoa  yeye  mwenyewe  kama  kafara  kwa  ajili  ya  kusimamisha  maapizo  yake.

Basi  mzimu  wa  mwanamke  huyo  uliwatesa  wana  ukoo  huo  kwa  muda mrefu  sana.

 Kila mwanamke  aliekuwa  anazliwa  katika  ukoo  alikuwa  hapati  ujauzito.

Ilifikia  kipindi  ambacho  endapo  mtoto  wa  kike  aliEzaliwa  katika  ukoo  huo  atabeba  ujauzito  basi  hiyo  ilichukuliwa  na  wazee  kama  ishara  kwamba  mtoto  huyo  wa  kike  sio  mtoto  wa  ukoo  huo  yani  hajazaliwa  na  mwanaume  kutoka  kwenye  ukoo  huo.

VIFUNGO   VYA    UKOO
Vifungo  vya  ukoo  ni  mambo  ambayo  watu  kutoka  katika  ukoo  Fulani  hutakiwa  kuyafanya  au  hawaruhusiwi kuyafanya  kwa  sababu  ya  maagano  ya  kiroho  yaliyo  ingiwa  na  mababu  wa  ukoo  huo   kwa  ajili  ya  ukoo.

Maagano  haya  huwajumuisha  na  kuwafunga  wana  ukoo  wote  kuanzia  walio  kuwa  hai  wakati  maagano  yanaingiwa  hadi  watakao  kuja  kuzaliwa  katika  vizazi  na  vizazi.

Maagano  hayo  huendana  na  masharti  maalumu  ambayo  ili  agano  liendelee  kusimama  basi watu  wa  ukoo huo  ni  lazima wayatimize.

Masharti  haya  ndio  ambayo  hujulikana  kama  miiko.
Kila  mtu  anaezaliwa  katika  ukoo  huo  hutakiwa  kutunza  na  kuheshimu  miiko  hiyo  na  endapo  ataenda  kinyume  basi  atapata  adhabu  ambayo  iliwekwa  wakati  maagano  yanaingiwa.

Mfano  kuna  baadhi  ya koo  kwao  ni  mwiko  kutoa  mimba .  Mwanamke  yoyote  yule   aliezaliwa  katika  koo  hizo  haruhusiwi  kutoa  ujauzito  hata  wa  wiki  moja  na  mwanamke  yoyote  yule ambae  atabeba  ujauzito  wa  mwanaume  ambae anatoka  katika  ukoo  huo  pia  haruhusiwi  kutoa  ujauzito.

Mwanamke   yoyote   kutoka  katika  ukoo  huo   ambae  atathubutu  kutoa  mimba  basi  atakufa .

Na  mwanamke  yoyote  atakae  toa  ujauzito  wa  mwanaume  anae  toka  katika  ukoo  huo  atakufa  endapo  atajaribu  kutoa  ujauzito  huo.

Hijalishi   unafahamu  ama  haufahamu  kuhusu  muiko  huu  endapo  utaukiuka  basi  utakufa  ilimradi  tu  upo  katika  ukoo  huo.

Kwa  ufupi  tofauti  kubwa  kati  ya  madeni  ya  ukoo  na  vifungo  vya  ukoo  ni  kwamba  madeni  ya  ukoo  haya  ni  mapigo  ambayo  kila  mtu  anaezaliwa  ndani  ya  ukoo  Fulani  ni  lazima  ayapate  kama  malipo  ya  kisasi  cha  mizimu wa  ukoo  dhidi  ya  wana  ukoo  huo  kwa  sababu  ya  maagano  ambayo  mababu  wa  ukoo  huo  waliyaingia  na  mizimu  hao  na  kuyavunja.

Lakini  vifungo  vya  ukoo  ni  miiko  ambayo  kila  mwana  ukoo  wa  ukoo  Fulani  anatakiwa  kuifuata  na  endapo  asipo  ifuata  au  endapo  ataivunja  basi  atapata  mapigo  Fulani.

Mtu  anaweza  kujiepusha  na  vifungo  vya  ukoo   kwa  kufuata  miiko  ya  ukoo  wake  na  kutoivunja  lakini  madeni  ya  ukoo  hawezi  kujiepusha  nayo  kwa  sababu  tayari mababu  zake  walikwisha  fanya  makosa hivyo  analipia  madeni  ama  makosa  ya  babu  zake.

Mtu  anaweza  kujiepusha  na  madeni  ya  ukoo  kwa  kuvunja  maagano  ambayo  babu  zake  waliingia na mizimu wa  ukoo.

VIPI  KUHUSU  MADENI  YA  FAMILIA ?
Kama  ilivyo  kwa  koo, familia  nazo  huwa  na  madeni ingawa  madeni  ya  familia  huwa  tofauti  kidogo na  madeni  ya  ukoo.

Tofauti  yake  ni  moja  ni  kwamba  madeni  haya  ya  wanafamilia  huwa  gusa  watu  wa  familia  peke  yake. Hayavuki  nje  ya  familia.

 Mwanafamilia  hii  anaweza  kuwa  na  madeni  ya  ukoo  lakini  wakati  huo  huo  anakuwa  na  madeni  ya  familia  ambayo yanamuhusu  yeye  na  wanafamilia wenzake  lakini  hayawahusu  wana ukoo wake.

 Mfano.  A  na  B  ni  mtu  na  kaka  ake. A  na  B  wanatoka  UKOO C ambao  una  madeni  ya  ukoo  au  vifungo  vya  ukoo  ambavyo  A  na  B  wanatakiwa  kuvilipa.

Wakati  huo  huo  A  ana  familia  yenye  mke  na  watoto  watano. A  ana  madeni  ya  familia . Madeni  ya  A  hayamuhusu  B hata  kidogo  wala  watoto  wa  B  ila  yanamuhusu  A  na  watoto  wa  A.

MADENI  YA  FAMILIA  NI  NINI  ?
Madeni  ya  familia  ni mapigo  ambayo  huwaandama  na  kuwapata  watu  kutoka  familia  Fulani  kwa  sababu  ya  makosa  yaliyo  fanywa  na  wana  familia  hao  eidha  wote  kwa  pamoja  au  asilimia  kubwa  ya  wanafamilia  hiyo  au  viongozi  wa  familia  hiyo.

Mfano : Kuna  pigo  moja  ambalo huwaandama  sana  wanawake  wanao  toka  katika  familia  za  watu  wenye  uwezo  .

Pigo  hili  lina husiana  na  WADADA  WA  KAZI  ZA  NYUMBANI  ama  MAHAUSIGELI.

Familia  inayo  wanyanyasa wadada  wa  kazi ijue  inapanda  mbegu  mbaya  sana  ya  kiroho  kwa  watoto  wa  kike  kutoka katika  familia  hiyo.

Watoto  wa  kike  kutoka  katika  familia  zinazo  watesa  na  kuwanyanyasa  mahausigeli  huwa WANANYANYASWA  SANA  KATIKA  NDOA  ZAO.

Haijalishi  wadada  hao  walishiriki  au  hawakushiriki  katika  kuwatesa  na  kuwanyanyasa  mahausigeli  hao  lakini wanapo  ingia  kwenye  ndoa  zao  huwa  WANATESWA  NA  KUNYANYASIKA  SANA.

Nikiwa  kama  tabibu  wa  tiba  za  jadi  nimekutana  na  kesi  kama  hii  nyingi  sana. Kama wewe  una  mdada  wa  kazi  nyumbani  kwako. Basi  jitahidi  kuishi  nae  vizuri.  Usimtese wala  kumnyanyasa  kwani  kwa  kumfanya  hivyo  unakuwa  umekopa  deni  ambalo  malipo yake  atakuja kuyalipa  mtoto  wako  kwa  mume  wake  pindi  atakapo kuja  kuolewa.

Mfano  mwingine  wa  madeni  ya  familia ni  pale  mama  anapo  muondoa  baba  ili  aweze  kurithi  mali.

Hili  ni  kosa  kubwa  sana  katika  ulimwengu  wa  rohoni.

 Watoto  wa  kike  walio zaliwa  katika  familia  hii  huwa  hawaolewi  kabisa  na  ikitokea  wameolewa  basi  ndoa huvunjika  ndani  ya  muda  mfupi  sana.

 Mwanamke  anapomtoa  mumewe  ili  arithi  mali  maana  yake  katika  ulimwengu  wa  rohoni  ni kwamba  familia  hiyo  haihitaji  mume.

Wao  wanachohitaji  ni  mali  tu . Hakuna  mume  atakae ingia  ndani  ya  familia hiyo. Kama pesa  wanaweza  kupata  pesa  nyingi sana, kama  mali  wanaweza  kupata  mali  nyingi  sana  lakini   waume  hawawezi  kupata  kwa  sababu  waume  hawatakiwi  katika  nyumba  hiyo.

Hiyo  ni  mifano michache  lakini  ipo  mifano  mingi  sana.  Tugusie  kidogo  kwenye  madeni ya  nafsi.

VIPI  KUHUSU  MADENI  NAFSI ?
Haya ni  mapigo  anayo  yapata  mtu  kutokana  na  mambo  mabaya  ambayo  ameyafanya  yeye  mwenyewe, maneno  ambayo  amejitamkia  yeye  mwenyewe  , jina  alilo  jiita  yeye  mwenyewe  au  jina aliloitwa  na  wazazi  wake.

Mambo  mabaya  ambayo  mtu  anakuwa  ameyafanya  yeye  mwenyewe  ni  pamoja  na  kuwadhulumu  yatima na  wajane, kuwafanyia  dhihaka  walemavu, kuvunja  agano  ambalo  ameliingia  yeye  mwenyewe  nakadhalika.

Maneno  ambayo  amejitamkia  yeye  mwenyewe  ni  maneno  yote  ambayo  mtu  anakuwa  amejitamkia  yeye  mwenyewe  kwa  mfano. Kuna  watu  huwa  wanajitamkiaga  maneno  mabaya  wao wenyewe  na  mwisho  wake  maneno  hayo hugeuka  kuwa  madeni  ambayo  hutakiwa  kuyalipa.

Kwa  mfano  mwanamke  yupo  kwenye  ndoa , halafu  baada ya  kutokea  kutokuelewana  kidogo  na  mume  wake  unamsikia  akisema “ Hii ndoa  hii, ipo  siku ntaondoka  tu  hapa. Yaani  we  ngoja  tu  ipo  siku nitaodoka  “  Mwisho  wa  siku  mwanamke  huyo  huondoka  katika  nyumba  hiyo ila  hata  sababu  yoyote  ya  msingi.

Mfano  mwingine unakuta  mtu  anasema  “ Ukitaka  kufa  mapema  wewe  tembea  na  mke  wa  mtu  tu “  halafu  baada  ya  muda  Fulani  anaingia  katika  mahusiano  na  mke  wa  mtu.

Hilo  ni deni  la rohoni  ambalo  lazima  alilipe. Mtu  huyo kweli  atakufa  kama  alivyo  kiri  mwenyewe.

Deni  la  jina  alilo  jipa  mwenyewe  au  jina  alilo  pewa  na  wazazi  wake.  Jina  la  mtu  ni  tamko  rasmi  kuhusu  maisha  ya  mtu  huyo, Ukimuita  mtoto  wako  jina  BARAKA  maana  yake  ni  kwamba  umemtamkia  na  kumnenea  Baraka  katika  maisha  yake.  Lakini  ukimuita  jina  mateso, msumbuko, au matatizo  jua  hilo  ni  deni  tayari  ambalo  lazima  alilipe  katika  maisha  yake.

Kuwa makini  sana  unapo mpa  mtoto  wako  jina.

VIPI   KUHUSU   MADENI  YA  MAENEO.
Kila  kijiji  kila  mtaa  kila  mji  au eneo vinaongozwa  na  kutawaliwa  na  roho maalumu.  Vijiji  na miji  ilipokuwa  inaanzishwa  wazee  walifanya  matambiko  maalumu  kwa  ajili  ya  kuingia  maagano  maalumu  na  viumbe  wa  kiroho  kwa  ajili  ya  kuutawala  na  kuulinda  mji  huo.

Unapo enda  kutafuta  maisha  katika  mji  Fulani  kitu  cha  kwanza  unacho  takiwa  kujua  ni  roho  zinazo  tawala  mji  huo ili uweze  kuendana  nazo.

Kuna  maeneo  mengine  yana  madeni  ya  kiroho  ambayo  kila  mtu  anaeishi  katika  eneo  hilo  ni  lazima  ayalipe.

Ndio  maana  unaweza  kuta  maeneo  mengine kijiji  kizima  au  mtaa  mzima  au  kata  nzima  hakunaga  mtu  alie  fanikiwa au hakuna  mtu  aliyesoma.  Wote  wanaishi  maisha  yanayo  fanana na  kila  anae  jaribu  kuinuka  anashushwa.

Ukienda  kuanza  maisha  katika  mji  Fulani  kitu  cha  kwanza  kabisa  unachotakiwa  kukijua  ni roho  zinazo  tawala  katika  mji  huo. Hii  itakusaidia  kujua  ni  kwa  namna  gani  utaweza  kufanya  biashara  au  kutafuta  maisha  katika  eneo  hilo.

Ukiona  hauwezi  kufanya  hivyo basi  chukua  ushauri  huu. Badilisha  jina  la  eneo  hilo. Jina  hilo  uwe  unalijua  wewe  mwenyewe  na  libebe  maono  yako. Kwa  mfano  unataka  kwenda  kuishi  katika  eneo  ambalo  watu  katika  eneo  hilo  huwa  hawafanikiwi, au  watoto  wote  wa  kiume  wanakuwa  mateja  na  wakike  wakuwa  machangudoa  au  wafanyabiashara  hawafanikiwi. Wewe  ukifika  hapo  kwa  mara  ya  kwanza  tamka  rasmi  kubadilisha  jina  la  mahali  hapo  na  kuliita  jina  ambalo  linaendana  na  kile  unacho  kitaka  katika  maisha  yako  au  kile  ambacho  umeenda  kukitafuta.

MWISHO  KABISA  NI  KUHUSU  MADENI  YA SIKU :  Haya  ni  madeni ambayo  husababishwa  na  wachawi  na  hukusudiwa  kulipwa  na  wakaazi  wa  kila  kijiji  na  kila  mtaa.

Kila  siku wachawi  wakiwa  wanawanga  usiku  kabla  hakujakucha  huwa  wanamwaga  dawa  kwenye  njia  panda  zinazo  ingia  katika  mitaa  na  vijiji  mbalimbali  na  kutamka  maneno  mabaya  dhidi  ya  wakaazi  wote  wa  eneo  hilo.

Maneno  hayo  ni  kama  vile :  WATU  WANAO ISHI  KATIKA  ENEO  HILI  WAKIENDA  KUFANYA  BIASHARA  WASIUZE, WANAO  TUMIA  VYOMBO  VYA MOTO  WAPATE  AJALI, WALIOPO  MAOFISINI  WAPATE  MATATIZO  OFISINI, WALIOPO  KATIKA  NDOA  WAPATE  MATATIZO  KATIKA  NDOA ..NAKADHALIKA  NAKADHALIKA.

Mambo  haya  hufanywa  kila  siku  kwa  usirias  mkubwa  sana. Yani  wachawi  wanapo  kuwa  wanawangia  watu  hufanya  hivyo  kana  kwamba  maisha yao  yanategemea  uwanga  huo.

Unashauriwa  kuwa  makini  sana.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA  MUNGWA  KABILI. ANAPATIKANA  KWA  SIMU  NAMBA  0744  000  473.

Unaweza  kupata  maarifa  Zaidi  kwa  kusoma  makala  zifuatazo:

1.     SABABU  ZA  KIROHO  KWA  NINI  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  HUWA  HAWAOLEWI…………………SEHEMU  YA  KWANZA.

https://ift.tt/2BuvsCL

2.     SABABU  ZA  KIROHO  KWA  NINI  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  HUWA  HAWAOLEWI…………………SEHEMU  YA  PILI


3.     JINSI  WANAWAKE  WAZURI  KUPITA  KIASI  WANAVYO  IBIWA  NYOTA  ZAO  NA  WANAWAKE  WENYE  UZURI  WA  KAWAIDA.