NEWS

16 Agosti 2018

WCB waongoza kuwania AFRIMA, Alikiba, Vanessa Mdee na Nandy Watoswa

Tuzo za All Africa Music Awards (Afrimma) za nchini Nigeria zimetoa list ya wasanii ambao wameingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Wasanii wengi wa Tanzania wameshindwa kufanya vizuri safari hii baada ya wasanii wa WCB   kutawala zaidi kwenye list hiyo.

Katika kipengele cha Best Male Artiste in Eastern Africa, Diamond, Raynanny pamoja na Harmonize wanachuana pamoja.

Kwa upande wa wasanii wa kike, Maua Sama amekuwa nominated kupitia kipengele cha Best Female Artiste in Eastern Africa.

Alikiba na Vanessa Mdee ni kati ya wasanii ambao wamekuwa wakitajwa mara kwa mara lakini mwaka huu wameshindwa kufurukuta kabisa.