NEWS

19 Septemba 2018

Madee: Dogo Janja na Irene Uwoya Hawajaachana

Hamad Ally ‘Madee’ (kulia) akiwa na Dogo Janja.

MKONGWE kunako gemu la Bongo Fleva, Hamad Ally ‘Madee’,  amefungukia uhusiano wa msanii mwenzake, Dogo Janja na mke wake staa wa Bongo Movie, Irene Uwoya, akisema wawili hao hawajaachana.

 

Madee ambaye ni baba mlezi wa Dogo Janja amezipiga chini tetesi hizo ambazo zimekuwa zikipamba moto kwenye mitandao ya kijamii.

 

Madee amedai na yeye mwenyewe anachangazwa na taarifa hizo kuzagaa mitandaoni, kwa watu kuongea masuala mengi juu ya ndoa hiyo bila ya kuwa na uhakika wa jambo husika.

Dogo Janja na Irene Uwoya hawajaachana nani amesema wameachana?, sidhani kama kuna kitu chochote kimewakuta ila ninachojua mimi wapo sawa, hadi dakika hii tunayozungumza na wapo pamoja kabisa”.

 

Siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa wanandoa Irene na Dogo Janja wanaelekea kupeana talaka baada ya kusemekana Uwoya kupata danga lenye pesa ndefu.

The post Madee: Dogo Janja na Irene Uwoya Hawajaachana appeared first on Global Publishers.