NEWS

15 Oktoba 2018

RATIBA YA KUAGA NA KUZIKA MWILI WA MTOTO WA MWAKASEGE

Ratiba ya Kumuaga mtoto wa Mwalimu Christopher Mwakasege, Joshua Mwakasege aliyefariki Alhamisi October 11 :-

 

Mwalimu atawasili Dar leo Jumatatu, Jumanne mwili utaagwa Mbezi Beach Lutheran Church, Jumatano alfajiri ni safari kuelekea Mbeya, na Alhamisi ni mazishi Tukuyu Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya.

 

Mahali ulipo msiba; Msiba uko Dar kwa mdogo wake Mwalimu Mwakasege anaitwa Eng. Mwakasingila (Mzee wa kanisa wa KKKT Mbezi Beach).

 

Jinsi ya kufika msibani; Fika hadi Mbezi Beach Jogoo, unaingia barabara ya Karibu Art Gallery kuelekea TAG Mbezi beach kisha utaona vibao vinavyoelekeza msiba ulipo.

 

Ratiba ya Jumatatu; Kutakuwa na sala ya pamoja na Mwalimu Mwakasege na familia yeke yote itakayofanyikia hapa msibani itakayoanza saa moja jioni, 7pm itakayoongozwa na Askofu , Mchungaji kiongozi na watumishi wengine.

 

Kuaga; Mwili wa marehemu utaagwa Jumanne 16 Oct kanisani KKKT Mbezi Beach Dar, kuanzia saa nane mchana (2pm), kaada ya kuaga mwili utapelekwa airport kwa ajili ya maandalizi ya safari.

 

Kusafirisha: Mwili utasafirishwa Jumatano 17 Oct kwa ndege

Mazishi: Yatafanyika alhamisi, Tukuyu, Mbeya 18 Oktoba,2018.

Muhtasari: Joshua alifariki ghafla baada ya kudondoka Alhamisi, Oktoba 11, 2018 akiwa kazini kwake World Bank Dar. Alikimbizwa Aga Khan hospital ila alifariki siku hiyo hiyo.

The post RATIBA YA KUAGA NA KUZIKA MWILI WA MTOTO WA MWAKASEGE appeared first on Global Publishers.