NEWS

29 Aprili 2019

Mbunge Ilemela aridhishwa na kasi ya ujenzi wa kivuko cha Bezi

Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa Kivuko cha kutoka Kayenze kuelekea Kisiwa cha Bezi unaoendelea katika karakana ya ujenzi wa vyombo vya majini chini ya Kampuni ya Songoro Marine ya jijini Mwanza.

Akizungumza mara baada ya kutembelea Karakana ya ujenzi wa Kivuko hicho kukagua hatua iliyofikiwa, Dkt Angeline Mabula amesema kuwa anaridhishwa na hatua ya ujenzi wa Kivuko hicho kilichogharimu shilingi Bilioni 2.7 mpaka kukamilika kwake sanjari na kumtaka mkandarasi wake kuhakikisha anakikamilisha kwa wakati ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi