NEWS

29 Aprili 2019

Rais Magufuli achangia Tsh. Milioni 2 Kwaajili ya Kununua Mashine

Rais John Magufuli amechangia Tsh. Milioni 2 kwa ajili ya kununua mashine ya kudurufu nakala pamoja na kuvuta umeme katika Shule ya Msingi Ileje iliyopo Rungwe mkoani Mbeya na kutoa siku 10 kukamilika kwa zoezi hilo.

Ametoa kiasi hicho baada ya wanafunzi wa shule hiyo kumlalamikia kutokuwa na umeme na kifaa hicho katika shule yao.

Rais Magufuli yupo mkoani Mbeya katika ziara yake ambap leo amezindua kiwanda cha parachichi katika muendelezo wa ziara yake ya siku nane mkoani Mbeya.