NEWS

25 Novemba 2019

Najua Nilikukosea Sana ila Naomba Umwache Huyo Mwanamke Unioe Mimi..Nitalea Mtoto Wake Kama wa Kwangu

Hivi wanawake ni watu wa aina gani? naombeni ushauri jamani, nilikuwa na mpenzi akanisaliti akaenda kuolewa na lijibaba nikatafuta mwingine, nimezaa nae mtoto mmoja natunaishi kwa furaha, cha ajabu yule alienikimbia ameanza kunitumia mesege, mojawapo imeandikwa hivi nanukuu
"Najua nilikukosea samahani sana ila naomba umuache huyo mwanamke, amin nitamlea mtoto wako kama wakwangu kumbuka unafahamika mbaka nyumbani familia yangu inanicheka kwa nilichokifanya"
Huyu mwanamke ninaeshi nae kaona hiyo massage kwenye simu yangu kaniambia kama nampenda nimsamehe yeye yuko radhi kuondoka....

Ukweli nilimpendaga sana alivyoniachaga nilipata hadi vidonda vya tumbo, niliposikia ameolewa ndo hata kazini nikawa siendi nikaishia kufukuzwa ila baada nikaja kumpata niliye nae sasa nikasahau machungu...sasa ndo  huyu anakuja tena katika maisha yangu , Im confused

Sasa Nifanyaje Nishaurini

By Silvester Limota