NEWS

12 Novemba 2019

Vurugu Alizofanya EBITOKE Mkutano wa Mlela...Meneja wa Hotel Adai ni Mpango Ulipangwa..Umesababisha Hasara Kubwa

Taarifa nyingine imeibuka baada ya Muigizaji **Ebitoke kusababisha vurugu kwenye mkutano wa Muigizaji Yusuph Mlela na waandishi wa habari uliofanyika leo Novemba 11 katika hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam.

Baada tukio hilo, alifuatwa Meneja wa hoteli hiyo, aliyejitambulisha kwa jina Suleiman Victor, ambaye alieleza kuwepo kwa mpango uliohisiwa kuhusishwa na tukio hilo lililosababisha hasara na uharibifu wa vitu kadhaa.

Meneja Suleiman alieleza kuwa Novemba 10, Mlela afika katika ofisi za hoteli hilo na kufanya
‘Booking’ kwa ajili ya mkutano huo na katika mazungumzo ya hapa na pale alinukuliwa katika maelezo kuwa kuna mchezo wataufanya.

Hata hivyo mpaka sasa haijabainika kama mpango huo ulilenga kufanyika kwa tukio hilo la vurungu inagwa katika maelezo ya juu juu, Yusuph Mlela alidai kuwa hakutegemea kama Ebitoke angefanya vurugu hizo.