NEWS

25 Septemba 2020

Sipo kwenye mahusiano ila natamani mwanamke- Marioo



Staa wa Muziki Nchini Tanzania Marioo amesema kuwa hataki kabisa kujiingiza kwenye Mapenzi kwasasa kwasababu anahofia kuumizwa .

Kupitia Kipindi Cha Refresh cha wasafi tv , Marioo amesema kuwa Kutokana na Ustaa wake , watu watashangaa sana kusikia ameumizwa kwenye Mapenzi hivyo hataki jambo hili litokee .


“Unajua mimi sitaki kukurupuka , unaweza ukajikuta unaimezwa alafu watu watashangaa sana kuona daah hadi marioo nae Kaumizwa” - alisema Marioo


Hata hivyo Licha ya kusema hajihusishi na Mapenzi kwasasa , Marioo amedai kwamba nae ana hisia na huwa anatamani wanawake Lakini anajitahidi Kujizuia .