Gari aina ya Toyota DYNA lenye namba za usajili 2330GX limepata ajali leo eneo la Kiuvyu katika barabara iendayo Chake Chake, Pemba, na kwa mujibu wa shuhuda wa ajali hiyo watu watatu wamejeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospitali ya Mkoani kwa matibabu. Chanzo cha ajali na majina ya majeruhi havikuweza kupatikana mara moja.