NEWS

7 Juni 2017

RAIS DK.SHEIN AJUMUIKA NA WAISLAMU KUMZIKA PROF.ISHAU



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alijumuika na Waislamu,Viongozi mbali mbali na Wananchi katika kumswalia Marehemu Mzee Prof.Ishau Abdalla Khamis katika Msikiti wa Ijumaa Donge leo,Marehemu aliwahi kushika nyazifa mbali mbali katika Serikalia ya Mapinduzi Zanzibar na Chama cha Mapinduzi.
1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Mkuu wa Mkoa Kaskazini Unguja,(wa pili mkushoto) pamoja na Viongozi wengine wakielekea katika kaburi wakati wa mazishi ya  Marehemu Mzee Prof.Ishau Abdalla Khamis yaliyofanyika leo kijiji cha Donge,Wilaya ya Kaskazini BUnguja.
2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto waliosimama) alijumuika na Waislamu,Viongozi mbali mbali na Wananchi katika mazishi ya Marehemu Mzee Prof.Ishau Abdalla Khamis katika kijiji cha Donge leo
3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein  akitia udongo katika kaburi la Marehemu Mzee Prof.Ishau Abdalla Khamis aliyezikwa leo katika kijiji cha  Donge,Willaya ya Kaskazini B Unguja,[Picha na Ikulu.]07/06/2017