Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira akisaini kitabu cha Wageni na baadaye kutoa pole kwa familia ya Marehemu Philemon Ndesamburo nyumbani kwake Kiboroloni, Moshi Mjini .
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira ameshawasili mkoani kwake tayari kwa kuanza kazi rasmi,ambapo leo ameanza majukumu yake kwa kukutana na kamati ya siasa ya Mkoa huo.
RC Mghwira akisaini kitabu cha Wageni kabla ya kuanza kuzungumza na kamati ya siasa ya mkoa wa Kilimanjaro mapema leo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,RC Anna Mghwira akisalimiana na viongozi mbalimbali wa kamati ya Siasa ya Mkoa,mapema leo
RC Mghwira akisalimiana na baadhi ya Wafanyakazi mara baada ya kuwasili nje ya ofisi yake,tayari kwa kuanza kazi kama Mkuu wa Mkoa mpya mkoani Kilimanjaro.