NEWS

6 Juni 2017

Uteuzi wa Anna: Zitto Aandamwa Mitandaoni, Aweweseka..!!!


Kutokana na uteuzi wa Mama Anna Mgwira aliyekuwa mwenyekiti wa ACT Wazalendo kuwa RC Kilimanjaro na mjumbe wa vikao vya CCM mkoa, Mh.Zitto Kabwe amekuwa akiandamwa mitandaoni na mashabiki wake.

Zitto amekuwa akilazimishwa kutoa tamko ikiwa pamoja na kukejeliwa kwamba ACT ni ''Amri ya Chama Tawala''. Lakini toka uteuzi huo Zitto Kabwe amekuwa aki-post nukuu za Quran jambo linaloonyesha kuweweseka kwake.