NEWS

31 Agosti 2018

Modric Mchezaji Bora Uefa

Luka Modric

KIUNGO wa Real Madrid, Luka Modric ame­fanikiwa kubeba Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi ya Mab­ingwa Ulaya katika utoaji wa tuzo ulio­fanyika jana.

 

Modric aliwazidi Mo­hamed Salah wa Liv­erpool na C r i s t i a n o Ronaldo wa Juventus al­iokuwa aki­wania nao katika na­fasi tatu za mwisho.

 

RAMOS USO KWA USO NA SALAH

Wakati utoaji wa tuzo ukiendelea, beki wa Real Madrid, Sergio Ramos alikuwa ame­kaa siti ya nyuma ya mshambuliaji wa Liver­pool, Mohamed Salah ambaye walitibuana wakati wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita.

Ramos alipita na kumgusa Salah be­gani wakati akitoka kuchukua tuzo, hali ambayo ilisababisha kamera nyingi kuwa­mulika wao, ikum­bukwe kuwa Ramos alimchezea faulo Salah ambaye alilazimika kukaa nje ya uwanja kwa miezi kadhaa na kushindwa kucheza hadi mwisho katika fainali ya Ulaya.

 

BECKHAM APATA TUZO

Staa wa za­mani wa Manchester United, David B e c k h a m alipata tuzo maalum ya Rais wa UEFA kutokana na m c h a n g o wake kwenye mchezo wa soka, am­bapo alikabidhiwa na kutoa hotuba fupi ya kushukuru.

 

TUZO NYINGINE

Mshambuliaji Bora: Cristiano Ronaldo

Kiungo Bora: Luka Modrić

Beki Bora: Sergio Ra­mos

Kipa Bora: Keylor Na­vas

The post Modric Mchezaji Bora Uefa appeared first on Global Publishers.