NEWS

31 Mei 2019

Mazishi ya Mama Yake, Isha Mashauzi Afunguka: Hajaniachia Nyumba Wala Gari! – Video

MWILI wa msanii Bi Rukia Jumaa ambaye ni mama mzazi wa mwimbaji maarufu wa Taarab, Isha Mashauzi umezikwa jana Alhamisi, Mei 30, 2019 nyumbani kwake Mbezi kwa Msuguri jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiwemo wasanii wenzake.

 

Akizungumzia msiba wa mama yake, Isha amesema chanzo cha kifo cha mama yake ni presha ambayo imekuwa ikimsumbua kwa muda mrefu sasa.

 

“Ahadi ya Mungu imetimia, kikubwa tumuombee mama apumzike mahali pema, hii ni safari ya kila mmoja wetu, tunachpaswa kuomba ni kuwa na mwisho mwema, kama kuna mtu alimkosea basi mimi mwanaye ninamuombea radhi, wamsamehe na kumuombea.

 

“Mama ameniachia upendo, siwezi kusema ameniachia nyumba au gari ama mali, kwa sababu vyote hivyo nitaviacha kama alivyoviacha yeye, lakini upendo aliyoniachia nitaondoka nao. Mama alikuwa mtu mwenye kukuleza ujapokosea, uwe mtoto wake au hata kama hajakuzaa, alipenda kutuelekeza maisha na namna ya kuishi duniani, alipenda sana dini,” amesema Isha.

Inalilah wainaillah rajiun!

The post Mazishi ya Mama Yake, Isha Mashauzi Afunguka: Hajaniachia Nyumba Wala Gari! – Video appeared first on Global Publishers.