NEWS

27 Novemba 2019

Alikiba Apata Tuhuma za Kutumia Maneno ya Wasanii Wenzake Bila Ruhusa, Ashauriwa Kuongeza Ubunifu – Video


Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Ali Salehe Kiba alimaarufu Ali Kiba amepata tuhuma za kutumia neno ambalo wasanii wenzake walikuwa wanalitumia kama alama ya kuwasaliana na mashabiki wao.

Wakiongea na Bongo5 wasanii wawili ambao wanafanya muziki pamoja Mandojo na Domokaya wameeza jinsi walianza kulitumia neno ambalo Alikiba analitumia huku wakidai alikiba analitumia bila ruhusa yao.

“Yeeh baba sisi tumeanza kuitumia muda sana na kila mtu anajua kuwa Yeeeh baba ni yetu, sasa Alikiba yeye kaichukua na kuanza kuitumia bila ruhusa yetu”

VIDEO: