NEWS

14 Novemba 2019

Mbunge aliedai Wahudumu wa ATCL hawana mvuto aomba Radhi Bungeni

Mbunge wa Kigoma Kusini (CCM), Mhe. Husna Mwilima leo Bungeni ameomba radhi shirika la Ndege ATCL  na Watanzania waliokwazika na kauli yake aliyosema Bungeni tarehe 7/11/2019 kwa kusema Wahudumu wa Ndege ya ATCL (Air hostess) hawana mvuto.

“Nataka nitanie kidogo, hizi ndege zetu zinafanya kazi nzuri lakini mle ndani hebu tuangalie wahudumu tunaowaajiri, tuangalie wahudumu ambao hata akigeuka abiria wanasema kweli tuna Air Hostess, sijui mnatumia vigezo gani? Unakuta Air Hostess mfupi, hana mvuto,” Alitoa Kauli hiyo  Alhamisi Novemba 7, 2019 wakati akichangia Mapendekezo ya Mpango wa Taifa wa Maendeleo bungeni jijini Dodoma.

Leo November 14, 2019 ameomba radhi bungeni na kusema;  “Nilitoa ile kauli lengo lilikuwa ni kuboresha shirika letu la Ndege la ATCL, kwa kuwa ile kauli yangu iliwaboa sana Watanzania hasa wanawake nitumie nafasi hii kuomba radhi Watanzania hasa wanawake wenzangu"