NEWS

30 Septemba 2020

Tembo 30 wa Zimbabwe 'Waliuawa na Bakteria



Maafisa wa wanyamapori nchini Zimbabwe wanashuku ugonjwa wa bakteria unaofahamika kama haemorrhagic septicaemia ndio chanzo cha vifo vya zaidi ya tembo 30 mwisho wa mwezi Agosti.

Sampuli zimetumwa ili kufanyiwa uchunguzi zaidi.

Tembo hao walipatikana wakiwa wamelala kifudifudi, hali ambayo wataalamu wanaashiria walikufa ghafla.

Wasimamizi wa mbuga za wanyama hawaamini waliuawa na wawindaji haramu, kwa sababu hawakutolewa pembe zao.