NEWS

24 Septemba 2020

Wakazi wa Temeke wengi hawana vitambulisho NIDA



Afisa Msajili vitambulisho vya Taifa katika Manispaa ya Temeke, Happines Gerald Minja ametoa tathmini fupi ya upatikanaji wa vitambulisho vya Taifa

Tathmini hiyo ni kwa wananchi wa Temeke ambayo inaonesha wananchi wengi hawajapata vitambulisho hivyo baada ya kutokidhi vigezo ikiwemo kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa.


“Wakazi wa Temeke idadi ni kubwa sana ambao hawana hivi vitambulisho jambo ambalo wengi wao limewaathiri hasa pale mtu anapohitaji kusafiri nje ya nchi”, amesema Minja.


Happines amesema wengine ambao wamekuwa hawana vitambulisho hivyo ni wale ambao walizarau pale walipotangaziwa juu ya kujiandikisha ili kupata kitambulisho cha taifa.