NEWS

2 Oktoba 2020

Polisi Yasitisha Wito kwa Lissu Yasema Aendelee na Kampeni

 


POLISI Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo Ijumaa Oktoba 2, 2020, imesitisha wito wa kumtaka mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu,  kufika kituo cha polisi na badala yake aendelee na ratiba za kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.