NEWS

1 Oktoba 2020

Waliokamatwa Kwa Mauaji ya Kada wa CCM Njombe Wakiri Kutenda Kosa

WATU wanne ambao wametiwa mbaroni kutokana na mauaji ya kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Njombe, Emmanuel Mlelwa, wamedaiwa kukiri kutenda mauaji hayo  kwa mujibu wa upelelezi wa polisi.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka,  na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mashtaka, imewataja watu hao kuwa ni Thadei Walter Mwanyika, George Sanga, Optatus Nkwera na Goodluck Oygen Mfuse.