Diamond Platnumz akihojiwa Nchini Nigeria katika Redio za The Beat Fm
Akiongea na Millard Ayo kupitia Top 20 ya Clouds Fm, Diamond amesema aliamua kusaini na kampuni ya simu ya MTN na kuwapa Exclusive ili apate pesa nyingi zaidi.
“So Inshallah pia naweza nikarudi na visenti vyangu ambavyo nilisaini…nilisaini na MTN peke yake kwasababu nilitaka kuwapa exclusive ili nipate pesa zaidi”.
‘Number 1′ (original) pia ilimpa dili nono Diamond hapa nyumbani ya kusaini Exclusive na Vodacom Tanzania ili kuuza kama muito wa simu Tanzania mara baada ya kutoka mwaka jana.
