NEWS

7 Juni 2017

Anna Mghwira: Mpaka sasa mimi ni Mwenyekiti wa Chama

"MPAKA sasa mimi ni mwenyekiti wa chama, nitakaa na wenzangu tuangalie mazingira ya chama chetu jinsi kilivyo kutokana na majukumu yangu nitakuwa Kilimanjaro kwa muda mwingi uwenyekiti wangu itakuaje"

Ni kauli ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Anna Mgwira alipokuwa kwenye mahojiano na Azam Tv jana mara baada ya kuapishwa kwenye nafasi ya ukuu wa Mkoa huo, ambapo amesisitiza kuwa yeye bado ni Mwenyekiti wa Chama cha Act-Wazalendo.

amesema kuwa uenyekiti wa chama chochote nchini ni shart uwe  Makamu Mwenyekiti Bara na Zanzibar na makamu wangu wote wanaimudu nafasi ya umakamu.

" Ilani ya chama cha mapinduzi ni lazima niitekeleze, napotekeleza Ilani nikiona ina mapungufu namuona Mwenyekiti wa chama na Katibu wake kwamba Ilani hii haitekelezeki.
"Wakati mwingine hizi Ilani watu wanaongea tu maneno hawazisomi, Ukiisoma Ilani ya kila chama cha Tanzania zote ni nzuri,"