SHEREHE ya maandalizi ya kumpokea mtoto wa msanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ambayo hujulikana kama’baby shower’ ilikuwa na kila ainaya shamra ambapo wasanii mbalimbali wa Bongo Muvi walifika kumpa sapoti ya aina yake usiku wa kuamkia leo.
Tukio hilo limefanyika katika ukumbi wa Afrika House Lounge uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Katika hafla hiyo ‘Gigy Maoney’ alionekana akimpongeza msanii wa Bongo Muvi, Jaqueline Wolper, akisema kuwa nguvu zake zimewezesha hafla kufanyika kwani hata vazi alilokuwa amelivaa alivalishwa na yeye.
Wasani wengine waliohudhuria hafla hiyo ni, Queen Darleen, Tunda, Hamisa Mobeto na wengine kibao.
The post ‘BABY SHOWER’ YA GIGI MONEY USIPIME! appeared first on Global Publishers.