NEWS

15 Agosti 2018

Kimenuka...Mbosso wa WCB Amtaka Rich Mavoko Atoe Ushahidi wa Kunyonywa WCB


Msanii kutoka WCB mbosso amefunguka kwa waandishiwa habari na kusema kuwa msanii rich  mavoko ambae amekuwa akitangaza kuwa WCB wanafanya kazi ya unyonyaji kwa wasanii wao ni uongo na kama kweli basi aje na kitu cha kuthibitisha maneno yake kama ni kweli.

Mbosso anasema kuwa kwa muda wote aliokuwa akifanya kazi wasafi mpaka sasa anaona kabisa kuwa hajarudisha hata robo ya kile alitakiwa kukirudisha kwa mambo ambayo amefanyiwa na WCB kwa muda wote.

mimi tangu nianze kuingiza kaz wasafi, sinaona kama nimerudisha mema niliyofanyiwa na WCB,  ile ela waliyowekeza kwangu bado sijarudisha hivyo nikiambiwa kuwa nina nyinya kwakweli binafsi nitakata kwa sababu naona mimi ndio ninawanyinya wao.

kwaio unaponiambia kuwa Mboso unanyinywa WCB basi uje na ushaidi kuwa nina nyonywaje.

Wasafi ina wasanii wengi sana ambao wamekuwa wakifanya kazi chini ya lebo hiyo lakini, Rich ni msanii wa kwanza kutoka WCB huku akisema kuwa sababu kubwa ni unyonyaji unaofanya na wasafi katika kufanya kazi na malipo lwa wasanii wao.