NEWS

3 Oktoba 2019

Uchaguzi Nafasi ya Mbowe, Msajili Aipa Chadema Siku 7

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania amekiandika barua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akikitaka kutoa maelezo kwa nini kisichukuliwe hatua kwa kutokufanya uchaguzi wa viongozi wake.

 

Barua ya Msajili iliyoandikwa Oktoba 1, 2019 na kusainiwa na Sisty Nyahonza kwa Niaba ya Msajili wa Vyama vya Siasa inasema uongozi wa Chadema chini ya Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe umemaliza muda wake tangu Septemba 14, 2019.

 

Katika barua hiyo, msajili amekitaka chama hicho kutoa maelezo hayo kabla ya Oktoba 7, 2019 saa 9:30 mchana.

The post Uchaguzi Nafasi ya Mbowe, Msajili Aipa Chadema Siku 7 appeared first on Global Publishers.