NEWS

3 Septemba 2020

Rihanna afunguka kwa mara ya kwanza juu ya urafiki wake na Chriss Brown



Mwanamuziki kutoka Marekani Robyn Rihanna Fenty maarufu Rihanna (32) amefunguka kwa mara ya kwanza juu ya urafiki wake na aliyekuwa mpenzi wake Chriss Brown (31)

Ikumbukwe, wawili hao wamewahi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi ambapo hayakuisha vizuri baada ya #ChrisBrown kumpiga #Rihanna na kumuachia makovu kadhaa mwilini mwake. Ilielezwa.


Akizungumza kwenye session mpya ya podcast ya Oprah, ‘Supersoul Conversations’ #Rihanna amefunguka kuwa yeye na #ChrisBrown wamendelea kuwa na maelewano mazuri tangu walipoachana.


“Tumekuwa tukiufanyia kazi urafiki wetu,” alisema Rihanna. “kwa sasa sisi ni marafiki wakubwa, tumejenga imani baina yetu na tunapendana sana na huenda tutapendana milele,” aliongeza Rihanna @badgalriri


“Kiukweli ninampenda, alikuwa mpenzi wa maisha yangu na nafahamu alinipenda pia ila ninafurahi ana amani maana sitakuwa na amani kama hana amani,” alimaliza Rihanna.