NEWS

13 Agosti 2021

Mwenyekiti wa Kampuni za Asas Group, Alhaj Faraj Ahmed Abri Afariki Dunia


Mwenyekiti wa Kampuni za Asas Group, Alhaj Faraj Ahmed Abri amefariki dunia leo Ijumaa Agosti 13 alfajiri, akiwa jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika familia hiyo, Mzee Abri atazikwa leo baada ya Swala ya adhuhuri katika makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.

"Hakutakuwa na mikusanyiko kwa tutakaokuwa Iringa, tafadhali tutumie zaidi teknolojia za habari kutoa pole na shughuli nyingine," imeeleza taarifa hiyo.