Kiungo Reus ana thamani ya Pauni Milioni 29.4 Borussia Dortmund.
Lakini inafahamika mambo yamebadilika tangu Bayern Munich ionyeshe nia ya kutaka kumsajili Mario Gotze.
Wasaka vipaji wa United wakuwa wakisaka mchezaji wa kiwango cha dunia kwa nafasi yoyote.
Pamoja na hayo, kiungo huyo anabakia kuwa chaguo lao la kwanza, ingawa pia wanasaka na washambuliaji, beki wa kushoto na beki wa kati waje kuwa warithi wa Patrice Evra na Rio Ferdinand mwishoni mwa msimu.