NEWS

5 Septemba 2020

Picha za Alikiba na mkewe zazua gumzo



Hizi hapa ni 'updates' kutoka kwa watu na mashabiki wa jamhuri ya mtandao wa Instagram baada ya staa Alikiba kupost picha ya pamoja akiwa na mkewe na mzazi mwenziye Mama Keyaan baada ya kupita miezi mitano.

Sasa kwenye picha hiyo ambayo imepostiwa kwenye ukarasa wa Alikiba imeleta comment nyingi ndani ya muda mfupi kutokana uwepo wa mkewe baada ya taarifa za wambea na wanamitandao zikieleza kuwa wawilio hao wameachana kisa kuishi mbalimbali.

Hizi hapa ni baadhi ya comments za mashabiki hao "Picha ya nne imekuheshimisha sana anko" 

"Nimefurahi kuona umeongozana na mkeo, That is nice of you" 


"Alikiba unajua unamke mzuri sana, blessed"


"Pisi kali ya Alikiba, wambea wataweka wapi sura zao" 


Ikumbukwe mara ya mwisho Alikiba kuonekana na mkewe ilikuwa kwenye Birthday ya kuzaliwa kwa mtoto wao Keyaan siku ya Februari 24, baada hii ya leo unaweza kusema 'RIP' kwa wambea wote ambao walikuwa walidhani wawili hao wameachana.